HAKIKA KIPUMBWI SATELLITE CITY NI KIUNGO MUHIMU KATIKA KUBORESHA BIASHARA YA UTALII NCHINI
Ni Mradi wa kimkakati unaounganisha Tanga kwa kilometa 80, Dar es Salaam kwa kilomita 180 na kilomita 60 tu hadi Zanzibar. Viwanja vimepakana na barabara mpya ya Lami ya Tanga-Pangani-Kipumbwi-Bagamoyo mpaka Dar es Salaam. Ambapo kukamilika kwa barabara hiyo itapunguza safari ya Tanga-Dar es Salaam kwa takribani kilometa 90.
Hii itapelekea idadi kubwa ya magari kuhama toka barabara ya Segera. Pia viwanja vipo km 3 tu toka Bandari ya Kipumbwi ambapo kunajengwa soko la Samaki na kiwanda cha kukaushia dagaa cha shilingi bil. 1.3.Hivyo vinaufanya Mji wa Kipumbwi kukua haraka na kuwa kitovu kipya cha uchumi wa buluu, biashara, usafirishaji, uvuvi, bandari na watalii wanaotoka Zanzibar, Mbuga ya Saadan na Kisiwa cha Maziwe.
Aidha mradi huu Kupitia vivutio vilivyosahaulika Mkoani Tanga{Magofu ya Tongoni na Pangani, Makaburi ya vita ya kwanza ya dunia Usagara, shule ya Kwanza ya Mkoloni Magila na Safu ya Milma ya Luhoto na Amani} unaunganisha watalii na uwanda mkuu wa vivutio vya Utalii Kaskazini{Mlima Kilanjaro, Serengeti, Ngorongoro, Manyara na venginevyo vingi}.
UTARATIBU WA KUPATA VIWANJA
1. Mteja atachagua kiwanja kupitia ramani atakayopatiwa na kampuni.
2.
Mteja
atafanya booking kwa kujaziwa fomu kwa gharama ya shilingi 20,000.{malipo ya
awali yafanyike ndani ya siku 7 kinyume chake kiwanja kitaacha huru kwa mteja
mwingine}
3.
Mteja
anaruhusiwa kufika site au kutuma mwakilishi kuhakiki eneo lake alilolichagua
{ndani ya muda wa booking}
4.
Mteja
ana nafasi ya kubadilisha kiwanja iwapo hatoridhika na eneo alichochagua na kulilipia
kabla ya kufika site.
5.
Malipo
yote yatafanyika kupitia akaunti ya Kampuni
6. Baada ya kufika site kwa gharama za mteja huduma ya kutembelea na kuonyeshwa maeneo Kipumbwi inatolewa kila siku na muda wote na Kampuni
7. Mteja
atatakiwa kuwasilisha nyaraka za uthibitisho wa malipo ya banki na kupewa
risiti ya kampuni.
8.
Iwapo
mteja atalimbikiza malipo ya miezi miwili na kuendelea pasipo kutoa taarifa na
kuidhinishwa na kampuni mteja atapoteza sifa yakuendelea kubaki na kiwanja
hicho na kitapatiwa mteja mwingine.
9.
Ikiwa
mteja atashindwa kuendelea na malipo anatakiwa kutoa taarifa kwa kampuni ili
kiwanja chake kiuzwe kwa mteja mwingine na pesa itarejeshwa baada ya miezi 8 na
itakatwa asilimia 20 ya usumbufu.
10.
Baada
ya kukamilisa malipo mteja atajaza fomu namba 19 ya maombi ya kumiliki ardhi
sambamba na fomu ya kampuni yakuthibitisha kukamilisha malipo na atawasilisha
nakala ya nida Pamoja na picha mbili kwa kila kiwanja.
11. Kampuni itamsaidia mteja kufungua akaunti ya maombi ya kumiliki ardhi{E-ardhi} Pamoja na ufuatiliaji wa hati miliki.
12. Mteja atawajibika kulipia kodi ya ardhi na gharama nyingine za maandalizi ya hati kwa serikali